Wadada wa kazi walitia timu wakiwa sambamba na mabosi zao.Kubwa ilikuwa kuwakabidhi zawadi zao washindi.
Mkurugenzi wa Primetime Promotion Juainna Kusaga alikuwepo kutoa sapoti katika tukio.
Tulikuwa na mgeni rasmi naibu waziri wa kazi,ajira na vijana mh.Makongoro Mahanga.
Pia alikabidhi zawadi,mwaka huu mshindi ilitakiwa awe mmoja kama mwaka jana na angejiondokea na Tsh ml 5 kamili.Baadae likaja wazo la kuanzisha category tatu ili igawanywe kwa washindi wa tatu.
Washindi wa tatu wa kwanza kila mmoja aliondoka na ml 1.5 na wengine kuondoka na elfu 80 kama asante ya kushiriki katika shindano.
Msosi time
Wadada waliserebuka kweli nyimbo kutoka Odama Band iliyokuwa ikipiga live
Na dada Subeth
Wasanii waliofanikiwa kuja ni pamoja na Linex,asante sana kwa kuja.
Barnaba alikuwa ana kazi ya harusi lakini akasema atapita hata kuimba wimbo mmoja lakini aliimba nyingi tu.Asante sana baba Steven kwa muda wako.Pia Mwasiti na Ali nipishe nawashukuru sana sana!
Crew ya Clouds tv ilikuwepo kufanikisha sherehe kuruka live jana hiyo.Mliokuwa mkiangalia tv manyumbani natumaini mliona live kupitia clouds tv.
Pichani Dokta Cheni na Simalenga.Dokta cheni alikuwa na shughuli zake lakini aliziacha baada ya kumpa mwaliko huo.Wadada hawa ndio mashabiki wakubwa wa filamu na maigizo ya hapa nyumbani.Pia ndio wasikilizaji wakubwa wa miziki ya hapa nyumbani.Picha ni nyingi sana ila hizi ni kwa kifupi tu.






















































