BLOG HII INADHAMINIWA NA VODACOM.......KAZI NI KWAKO!!!

BLOG HII INADHAMINIWA NA VODACOM.......KAZI NI KWAKO

Monday, May 28, 2012

TULIVYOJIACHIA JANA NA DADA WA KAZI ZA NYUMBANI

 Hizi ni picha kwa ufupi za tukio la sherehe ya wadada bora wa kazi za nyumbani mwaka huu 2012.Sherehe hii tuliifanyia katika ukumbi wa Zhongua garden baada ya matengenezo pamekuwa pazuri kweli na uongozi ukiwa ni mpya.
 Wadada wa kazi walitia timu wakiwa sambamba na mabosi zao.Kubwa ilikuwa kuwakabidhi zawadi zao washindi.



 Mkurugenzi wa Primetime Promotion Juainna Kusaga alikuwepo kutoa sapoti katika tukio.
Galina na Godliver



 Tulikuwa na mgeni rasmi naibu waziri wa kazi,ajira na vijana mh.Makongoro Mahanga.
 Pia alikabidhi zawadi,mwaka huu mshindi ilitakiwa awe mmoja kama mwaka jana na angejiondokea na Tsh ml 5 kamili.Baadae likaja wazo la kuanzisha category tatu ili igawanywe kwa washindi wa tatu.
Washindi wa tatu wa kwanza kila mmoja aliondoka na ml 1.5 na wengine kuondoka na elfu 80 kama asante ya kushiriki katika shindano.
 Msosi time

 Wadada waliserebuka kweli nyimbo kutoka Odama Band iliyokuwa ikipiga live

 Na dada Subeth

 Wasanii waliofanikiwa kuja ni pamoja na Linex,asante sana kwa kuja. 
Barnaba alikuwa ana kazi ya harusi lakini akasema atapita hata kuimba wimbo mmoja lakini aliimba nyingi tu.Asante sana baba Steven kwa muda wako.Pia Mwasiti na Ali nipishe nawashukuru sana sana!

Crew ya Clouds tv ilikuwepo kufanikisha sherehe kuruka live jana hiyo.Mliokuwa mkiangalia tv manyumbani natumaini mliona live kupitia clouds tv.
Pichani Dokta Cheni na Simalenga.Dokta cheni alikuwa na shughuli zake lakini aliziacha baada ya kumpa mwaliko huo.Wadada hawa ndio mashabiki wakubwa wa filamu na maigizo ya hapa nyumbani.Pia ndio wasikilizaji wakubwa wa miziki ya hapa nyumbani.Picha ni nyingi sana ila hizi ni kwa kifupi tu.

Sunday, May 27, 2012

PICHA ZA FINALI YA DADA BORA WA KAZI ZA NYUMBANI

 Mimi sambamba na Gea Habib tuliwakutanisha wadada 9 walioingia hatua ya mwisho ya fainali.
Gea Habib
Tulikuwa tunatumia studio ya clouds tv
Tulianza na category ya kwanza ya dada wa kazi za nyumbani lakini anajiendeleza kimasomo,ufundi na ujasiriamali.Dada Harriety,Theo Gilla na Yoseti Brison.
 Na mshindi alikuwa..............
Dada Theo Gilla
Tukaingia category ya pili jamani hakuna category iliyokuwa ngumu kama hii yaani kila mmoja ana hadithi inayokugusa kwa wale mliosikiliza leo tena au kutazama clouds tv mtakubaliana na mimi.Pichani ni dada Asia,Leah Mkewa na Restuta ambae ndio aliibuka mshindi akitokea Mwanza.
Washiriki wa category ya dada bora wa kazi mchapakazi alikuwepo dada Happy Simon,Anna Antony,na Habiba Hamis wa Arusha.Na mshindi alikuwa dada Happy Simon wa kwanza pichani mwenye skirt nyeusi.
Hivi ndio ilikuwa ikionekanakupitia clouds tv
 Pia wageni wetu waliokuwa wameongozana na mabosi zao walipata nafasi ya kutembelea kila eneo ofisini kwetu clouds fm na kutambulishwa watu ambao wamekuwa wakiwasikia kwenye radio.
Shukrani za kipekee ziende kwa clouds tv crew
familiaMebu na George ambae alinisaidia sana mpaka usiku mwingi kwenda kurekodi  wanazoishi hawa madada kwa ajili ya tv production.
Crew ya makameraman na wote ambao walitia mkono katika hili asanteni sana,One love!
Leo jioni ndio tunakabidhi zawadi washindi wetu na sherehe fupi kufanyika pale Zonghua Garden.Watakaofika ni kwa mualiko maalum ila wengi ni wadada wa kazi na mabosi zao na wadau mbali mbali.

Thursday, May 24, 2012

JANA MBONI ALIZINDUA KIPINDI CHAKE CHA TV,THE MBONI SHOW

Ilikuwa ni Serena hotel wadau mbalimbali walikutana kumpa sapoti na kuangalia kipindi hicho.
Mboni na marafiki zake waliokuja kumpa sapoti.
Set up ya studio
Mboni akielezea juu ya kipindi chake na kuwashukuru wote waliofika kukiona kwa mara ya kwanza.
Hongera Mboni na kila la heri  NA THE MBONI SHOW wewe umedhihirisha kuwa tusiogope KUJARIBU KATIKA MAISHA.

Wednesday, May 23, 2012

SIKU NZIMA YA LEO NIMEKUWA NIKISILIZA WIMBO HUU!

Amini kwamba hakuna kinachoshindikana hapa duniani ni wewe kuamua tu.Dream big na hakikisha unafight kutimiza ndoto yako.Vikwazo na changamoto zipo ila pambana navyo ukianguka inuka na endelea kukimbiza ndoto yako....inawezekana to be the world greatest!

NINA WALINDA WATOTO WANGU KUPITILIZA,NAHISI NAKOSEA.NIFANYEJE??



Habari Dina,Niliwahi kuwasiliana na wewe kwa njia ya sms na nikakueleza
kuwa nina jambo ambalo nahitaji msaada,ukanipa hii email yako ili
nikuandikie,mimi kiukweli matatizo naona kama ninayo mengi ila
linalonisumbua ambalo nahisi linaweza kuwaletea matatizo wanangu ni
hili.Mimi kwa sasa ninawatoto watatu wa kwanza yupo darasa la nne,wa
pili yupo darasa
la tatu na wamwisho hajaanza.Nilipokuwa mdogo wa umri
kati ya miaka 6 au7 hivi nilishuhudia matendo ya udhalilishaji wa
kijinsia na pia mimi kutendewa nandugu zetu,unajua mambo ya extended
family mnaishi nyumba moja watu kumi na kitu,ishirini.Sisi tulipokuwa
tunaishi tulikuwa
wengi sana na wanaotuzidi umri walikuwa wasichana
dada zetu kama wanne na vijana kama watano na sisi watoto tulikuwa
wanne,unajua tena vijana wanapotaka kubalehe sijui huwa inakuwaje ila
hapo ndipo ilipotokea huo udhalilishaji ninaokwambia,Dina ni mambo
mengi sana na sijawahi kumwambia mtu ila sasanimepata familia naanza
kuona ile hali iliniathiri vipi,toka nimepata watoto sina amani kabisa
nawalinda watoto wangu kupitiliza,namhofia kila mtu,siwezi kukaa mbali
na wanangu hata kwa dk 1,kila anaewasogelea naona kama atawadhuru,sasa
imefikia hatua wanakua wanataka kucheza na wenzao mimi hata nikiruhusu
lazima niwe karibu yao,hali hii inanitesa maana naona huyu mkubwa
atakapoanza kukua itabidi apate uhuru na mimi kama nikiwa bado na hali
hii nahofia mwanangu atanichukia maana wakati yeye atakapokuwa anataka
kuwa na vijana wenzie mimi bado nitakataa kwa kuona kule
ataumizwa,sasa sijui niko sawa ninavyofanya au?mana nimeishaanza kuona
wanangu hawapapendi hapa nyumbani kila likizo wanataka waende kwa bibi
na babu yao,naomba unisaidie au ulifikishe kwa wadau wanipe mawazo.
Asante.
Tumpe mawazo mwenzetu maana naamini wengi tuna expirience mbalimbali za kifamilia kutokana na makuzi tuliyopitia.Si tu makuzi bali hali halisi ya maisha ilivyo.

MJENGONI LEO HII

Hii ilikuwa katika shooting ya kazi kadhaa za leo tena lakini kwa upande wa tv.